Contact us:

 

AVIC Consultants

Plot 60 Block 45, Kajenge Street, Kijitonyama,

P O Box 11924,

Dar es Salaam,

Tanzania

 

Phones

 

+ 255 752 447 689

 

Email Address

 

ajmwambola@tanbusiness.co.tz

SABABU YA KUANZISHA ONLINE TV

Kilicho sababisha wamiliki wa Tan Business Channel kuanzisha Online TV, ni baada ya kutambua kuna changamoto ya ajira, inayo wakabili vijana wetu

Vijana wetu wanao hitimu vyuo vikuu na vyuo vya kati, wanakabiliwa na changamoto ya kupata ajira kutoka sekta binafsi na serikalini.

Kutokana na hali hiyo, viongozi waTan Business Channel tumeamua kuanzisha Online TV, ili ifundushe elimu ya ujasiriamali kwa vijana wetu.

WALENGWA WA VIPINDI VYA TAN BUSINESS ONLINE TV

Tan Business Channel Online TV, inatangaza vipindi ambavyo vinakidhi mahitaji ya watazamaji tunao walenga  

Watamazaji tunao walenga ni vijana wenye umri kati ya miaka 18-35 ambao wanahitaji elimu ya ujasiriamali.

Matumaini yetu ni kuwa, elimu ya ujasiriamali watakayopata vijana wetu, itawasaidia kujiajiri wenyewe

VIPINDI VYA TAN BUSINESS CHANNEL ONLINE TV

Kuna aina 3 za vipindi vinavyo tangazwa na Tan Business Channel kama vifuatavyo:

· Kuanzisha biashara

· Kusimamia biashara

· Kutengeneza hesabu za biashara

KUANZISHA BIASHARA

Kipindi cha kuanzisha biashara, ni muhimu kwa kuweka misingi imara, wakati wa kuanzisha biashara

 

Iwapo biashara haitakuwa na misingi imara wakati wa kuanzisha, ni wazi kuwa hiyo biashara haitakuwa endelevu

 

Hali ya kusuasua kwa biashara kama itaendelea, kuna uwezakano mkubwa wa biashara kufilisika

KIPINDI CHA KUENDELEZA BIASHARA

Iwapo unafakiwa kuweka misingi imara ya biashara mpya, ni muhimu kufanikisha kuwa na biashara endelevu

 

Unaweza kuwa na biashara endelevu, kwa kuweka mfumo mzuri wa kusimamia biashara. Huo mfumo unatakiwa kufanikisha biashara kufanyika kwa ufanisi na faida inapatikana

KUTENGENEZA HESABU ZA BIASHARA

Huwezi kufanikiwa kuwa na biashara endelevu kama hutengenezi plan ya biashara na kufuatilia utekelezaji wake

 

Kupima ufanisi wa utekelezaji wa plan za biashara, kunahitaji utengenezaji wa taarifa za biashara

 

Moja ya taarifa za biashara ambayo ni ya muhimu, ni ya hesabu za biashara.

Taarifa ya hesabu za biashara inaeleza mambo muhimu yafuatayo:

· Kama biashara inapata faida au hasara

· Kama kuna mtiririko mzuri au mbaya wa fedha za biashara

· Kama kuna ongezeko au upungufu wa mali, madeni, faida na mtaji wa biashara

Usikose kuangalia kipindi cha Dira ya Ujasiriamali siku za Jumatatu-Jumamosi 9.00-10.00 PM

 

https://youtube.com/alimwambola

 

Pata elimu ya ujasiriamali kupitia Tan Business Online School

 

https://ali-mwambola-s-school.teachable.com/p/home

Pata kitabu cha ujasiriamali kupitia Draft 2 Digital

 

www.draft2digital.com

TAN BUSINESS CHANNEL ONLINE TV

TAN BUSINESS BOOK PUBLISHING

TAN BUSINESS ONLINE SCHOOL

Tan Business Channel